Biblia inaishia na picha yenye nguvu ya tumaini. Katika Ufunuo 21:23, tunaambiwa kwamba katika mbingu mpya na dunia mpya, hakutakuwa na haja ya jua wala mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu huipa nuru, na Mwana-Kondoo ndiye taa yake. Kwa wale wanaomwamini Yesu Kristo, huu ndio wakati wetu ujao. Mahali pazuri ambapo dhambi, mateso, na kifo havipo tena, na ambapo tutaishi mbele za Mungu milele. Tumaini hili linawezekana kwa sababu Yesu aliingia gizani mwa ulimwengu wetu, akafa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na akafufuka tena katika ushindi. Giza halikushinda. Yesu alishinda.
Lakini hadi siku hiyo, Mungu anatuita kuishi kama watu wa nuru wanaoshiriki tumaini la Injili na wengine. Tuwaambie wale walio karibu nasi kuhusu Yesu ni Nani na kile alichowafanyia!
________________________
Share Life Africa ni kipindi cha redio na podikasti cha Kikristo cha Evangelism Explosion International Africa Ministries; ambacho kimejitolea kukupa vifaa na rasilimali zinazohitajika ili kushiriki imani yako na wengine kwa ujasiri na kwa ufanisi.”