Sisi tulio viongozi wa kiroho mara nyingi huathiriwa na sauti za watu waliotuzunguka. Sauti za sifa, na sauti za malalamiko hufuatana na kiongozi yeyote siku zote. Lakini Biblia inasema nini juu ya sauti zile? Kama wafuasi wa Yesu Kristo, sisi tunapaswa kuishi kama watu waliosulibiwa. Kwa maneno mengine, tumtegee Mungu sikio letu na kutosikiliza sana sauti za watu aidha wanapotusifu au wanapolalamika juu yetu.
Create your
podcast in
minutes
It is Free